MozFest House: Kenya ni mkutano wa kikanda ambao utaleta pamoja wajenzi, watafiti, watunga sera, wanaharakati, mashirika ya kiraia, na uhisani ili waungane na kuchunguza masuala muhimu yanayohusiana na mtandao ulioboreshwa na AI inayoaminika. Jiunge nasi Nairobi, tarehe 21 hadi 22 Septemba 2023.

Jinyakulie tiketi yako

MozFest House: Kenya ni upanuzi wa kikanda wa MozFest, mkusanyiko wa kwanza wa wanaharakati, wasanii, wanateknolojia na waelimishaji katika harakati mbalimbali za kimataifa zinazopigania ulimwengu wa kidijitali unaozingatia masilahi ya kibinadamu. Likiendelezwa kutoka kwa MozFest House Amsterdam, hili litakuwa tukio la pili la MozFest House mwaka huu, lakini wakati huu, likilenga kanda ya Afrika Mashariki na Kusini.

MozFest House Amsterdam Stage with Presenter
53019463691_37a3a4dff2_c
53019461836_a3d6dc1f04_c

MozFest House ni nini?

Mwaka huu, MozFest House inawezeshwa na nguvu zetu za pamoja ili kuboresha mazingira yetu ya kidijitali, kujenga mifumo ya mabadiliko, na kudumisha kasi ndani ya jamii zetu kuelekea maendeleo mazuri ya haki za kibinadamu na za kidijitali.

Ni kupitia nguvu ya pamoja ya watu kwamba tunaweza kuhakikisha kuwepo kwa AI inayoaminika ili tuelekeze jitihada zetu kuelekea masuala muhimu kama vile upendeleo, uwazi, usimamizi wa data, na harakati ya kujenga.

Utakachotarajia kuona

MozFest House: Kenya ni mfano wa mkakati wa Mozilla unaoitwa Africa Innovation Mradi, unaowezesha nafasi kwa jamii mbalimbali kuja pamoja kutoa ujuzi, kujadiliana na kujenga ushirikiano unaozingatia maendeleo na usimamizi wa teknolojia ya kidijitali katika Afrika ya Mashariki na Kusini.

MozFest House: Kenya inalenga kusema ukweli wa mambo kuhusu uwezo wa usalama wa kidijitali, haki za kidijitali, uwajibikaji wa kiteknolojia na haja ya usimamizi wa mtandao. MozFest House inawaleta wenyeji pamoja. Tunakuja pamoja na washirika wa kikanda na sauti mpya ili kuchunguza masuala haya kutoka kwa mitazamo mbalimbali. Kikweli ni tukio la kila mtu katika jamii, hivyo kama wewe ni mwanateknolojia, mwalimu, mwanaharakati, msanii au mtunga sera, nyote mnakaribishwa!

Mazungumzo

Pata kufurahia mazungumzo ya kuchochea fikira na kuleta mazungumzo pamoja na viongozi wa jamii na maoni juu ya mwenendo wa mfumo ikolojia wa kidijitali na uvumbuzi unaoendelea katika Afrika ya Mashariki na Kusini. Hudhuria mjadala mkuu! Jishirikishe! Jadiliana na Hoji wataalamu!

Jinyakulie tiketi yako

Vikao vya ubunifu

Pata kuchochewa na ubunifu wa wazalishaji wa maudhui, wasanii, wajenzi, wabunifu na wajasiriamali wanaokubali kikamilifu teknolojia zinazohusika. Shirikiana na ujifunze kutokana na maonyesho mbalimbali na vikao vya mafunzo halisi kukiwemo na warsha na "hackathon" (tukio linalowaleta wasanidi programu za kompyuta pamoja).

Jinyakulie tiketi yako

Tukio la "The Barn"

Gundua mashirika mapya au shirikiana na wavumbuzi wapya, wanaharakati wa haki za kidijitali na washawishi na watunga sera katika mazingira tulivu kama ya shambani. Barizi palipo na hewa nyingi na nafasi ya kuanzisha ushirikiano huo!

Jinyakulie tiketi yako

Ratiba

Ratiba itatolewa Agosti na itajumuisha warsha kadhaa za ushirikiano na za kuvutia, majadiliano na midahalo, mitambo ya sanaa, tukio la usanidi wa programu za tarakilishi, na mengi zaidi! Ikiwa wewe ni msanii, mtunga sera, mhadhiri, mwanaharakati, teknolojia au mtu anayetumia teknolojia nyumbani au kazi, kuna kitu cha kuchunguza.

Jinyakulie tiketi yako
picha ya watu watatu wa kujitolea wakiwa wamevaa fulana za rangi ya chungwa ambazo zina nembo ya MozFest House

Je, wewe ni mwenyeji wa eneo la Nairobi na una nia ya kujiunga nasi ili uweze kusaidia kuleta MozFest House: Kenya?
Jisajili ili ujitolee →

© OpenCityMap
Eneo

MozFest House: Kenya is taking place at Shamba Events

Shamba Events is a peaceful retreat from the bustling Nairobi traffic, with plenty of fresh air. The barn, stables and vast lawns are Ideal for events of any kind. It is located 100 meters beyond the entrance to Shamba Cafe & Shop along Loresho Ridge, just before the entrance to the University of Nairobi/VetLab Campus.